Neno La Mungu Limewekwa Wazi

NENO LAKO NDIYO UKWELI. . . . " Yohana 17:17
"TENA MTAIFAHAMU KWELI, NAYO HIYO KWELI ITAWAWEKA HURU." Yohana 8:32

HITAJI LA WANADAMU LA WOKOVU
"Kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu." Warumi 3:23

Kutoka Mwanzo:
Adamu Na Hawa
* BUSTANI YA EDENI
* DHAMBI YA KUTOTII

HUKUMU: Kufukuzwa . . . Kazi . . . Maumivu. . . . Hatia

Dhambi ni URITHI

"Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu; Mama yangu alinichukua mimba hatiani." Zaburi 51:5
"Hakuna mwenye haki hata mmoja." Warumi 3:10
"Basi mwanadamu wa tabia ya asili” (ambaye hajaokoka) ”hayapokei mambo ya Roho wa Mungu. . . ." 1 Wakorintho 2:14


MWANADAMU HAWEZI KUJIOKOA MWENYEWE!

KAZI ZETU
"Si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu.” Tito 3:5

HAKI YETU
"Kwa maana sisi sote tumekuwa kama mtu aliye mchafu na matendo yetu yote ya haki yamekuwa kama nguo iliyotiwa unajisi. . . .”

WEMA WETU:
". . . Hakuna aliye mwema ni mmoja. . . .” Naye ni Mungu. Mathayo 19:17

DINI YETU:
"Kwa sababu hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki mbele zake kwa matendo ya sheria. . . ." Warumi 3:20

"Hali tukijua ya kuwa mwanadamu, hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo Yesu. . . ." Wagalatia 2:16

HAYAWEZI KUTUOKOA 
MUNGU PEKEE NDIYE NAYEOKOA 


KIPAWA CHA MUNGU CHA WOKOVU

KWA NJIA YA KRISTO:
"Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote...." Matendo 4:12

". . .Na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo." Waebrania 9:22

MTIRIRIKO WA DAMU

"Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu....” Isaya 53:5


SHERIA:

Mungu aliyompa Musa Mlima Sinai.

SHERIA ZA SHEREHE :
* MAKUHANI
* DHABIHU
* DAMU

KUELEKEZA KALVARI:
"Mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo. . . ." Wakolosai 2:17
"Hivyo torati imekuwa kiongozi kutuleta kwa Kristo. . . ." Wagalatia 3:24

SHERIA HAIKUWA YA KUDUMU
"Ni dhahiri ya kwamba hakuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu katika sheria. . . ." Wagalatia 3:11
"Kristo alitukomboa katika laana ya torati,. . . ." Wagalatia 3:13
"Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana. . .tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa. . . ." Luka 16:16



MWANA KONDOO :

YOHANA ALIMTAMBULISHA: “. . . Tazama Mwana-kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!" Yohana 1:29

ALIKUWA: ". . . Mwana-Kondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia." Ufunuo 13:8
". . . Astahili Mwana-Kondoo aliyechinjwa, kuupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka." Ufunuo 5:12

KUZALIWA KWAKE: KULITANGAZWA NA MALAIKA: "Maana leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi ndiye Kristo Bwana." Luka 2:11
MAISHA YAKE: ". . . Naye akazunguka huko na huko, akitenda kazi njema na kuponya wote walioonewa na Ibilisi. . . ." Matendo 10:38

ALISEMA: "Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima. . . ." Yohana 14:6
"Mimi ndimi mlango, mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho." Yohana 10:9
"Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake." 1 Petro 2:22

KIFO CHAKE: "Akatoka, hali akijichukulia msalaba wake, mpaka mahali paitwapo . . . Golgotha wakamsulubisha huko. . . ."
Yohana 19:17-18
". . . Kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi." Warumi 5:8

"YAMEKWISHA." Yohana 19:30
Kilio Kutoka Msalabani
Mpango wa Mungu Kuokoa

MAZIKO: “Naye . . . akamfungia ile sanda, . . . lililochongwa mwambani. . . ." Marko 15:46

UFUFUKO: “. . .Mnamtafuta Yesu . . aliyesulubiwa; amefufuka." Marko 16:6

KUPAA: ". . . Wingu likampokea kutoka machoni pao." Matendo 1:9



KANISA:
* KANISA NI USHIRIKA WA WAAMINI WALIOBAPTIZWA NA AMBAO WAMETII MPANGO WA WOKOVU WA MUNGU.
* KUNA KANISA MOJA TU: "MWILI MMOJA" Waefeso 4:4 "IMANI MOJA" Waefeso 4:5

LILIAHADIWA:
“... Na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda." Mathayo 16:18

SIKU CHACHE KABLA YA PENTEKOSTE ALIAHIDI: “. . . Bali ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu baada ya siku hizi chache." Matendo 1:5

LILIANZISHWA: "Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako . . . . Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajaliakutamka." Matendo 2:1-4

LILIFUNGULIWA:
". . .Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.” Matendo 2:38

"Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali. . . ." Matendo 2:39

KANISA LIKO WAZI: ". . . na yeye atakaye. . . ." Ufunuo 22:17


TUKIO:
Yesu alisema: ". . . Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuingia ufalme wa Mungu." Yohana 3:5

HAYA YALITAFSIRIWA NA KUELEZEWA KATIKA UJUMBE WA PETRO KATIKA MATENDO YA MITUME.

"Mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu." Matendo 2:38

WAYAHUDI: Matendo 2:4
"Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka."

WASAMARIA: Matendo 8:15-17
". . . Wakawaombea wampokee Roho Mtakatifu; kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao, ila wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu . . nao wakampokea Roho Mtakatifu."

MATAIFA: Matendo 10: 44-48
". . . Roho Mtakatifu akawashukia wote waliolisikia lile neno." (aya 44) Na wale waliotahiriwa, walioamini, wakashangaa, watu wote waliokuja pamoja na Petro, kwa sababu Mataifa nao wamemwagiwa kipawa cha Roho Mtakatifu. Kwa maana waliwasikia wakisema kwa lugha. . . . Ni nani awezaye kukataza maji, hawa wasibatizwe, watu waliopokea Roho Mtakatifu vile vile kama sisi? Akaamuru wabatizwe kwa Jina lake Yesu Kristo. . . ."

WATU WA DINI: Matendo 19:2-6
". . . Je! mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini? Wakamjibu, La. . . . " (aya 2) "Waliposikia haya wakabatizwa kwa jina la Bwana Yesu. . . . Roho Mtakatifu akaja juu yao; wakaanza kunena kwa lugha, na kutabiri."

TUKIO LA KUZALIWA UPYA LILIKUWA LA KUFANANA:
WOTE WALITUBU NA KUAMINI WOTE WAKABATIZWA KWA JINA LA YESU WAKAJAZWA NA ROHO MTAKATIFU NA KUNENA KWA LUGHA MPYA



". . . NITAMIMINA ROHO YANGU JUU YA WOTE WENYE MWILI... ." Yoeli 2:28



KWA NINI JINA LA YESU NI MUHIMU!

"Nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao." Mathayo 1:21
KWA KUJITAMBULISHA: SISI NI MALI YA NANI: “. . . Ambaye kwa jina lake ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa. . . ." Waefeso 3:14-15

KATIKA KIBIASHARA: JINA HUFANYA HUNDI NA HATI ZA BIASHARA KUWA HALALI NA KUFAA:
"Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu." Wakolosai 3:17

KATIKA NDOA: BIBI ARUSI HUKUBALI KUCHUKUA JINA LA MUMEWE:
". . . Mungu . . . alivyowaangalia Mataifa ili achague watu katika hao kwa ajili ya jina lake." Matendo 15:14

KATIKA WOKOVU: "Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa
maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo." Matendo 4:12

YESU: “YHVH . . . AMEKUWA WOKOVU WANGU.” Isaya 12:2
(Marejeo ya Maandiko Luka 1:77; 2:30; 3:6)

MUNGU ALIKUWA NA VYEO VINGI LAKINI KWENYE UKOMBOZI NI JINA MOJA TU.

"Naye BWANA atakuwa Mfalme juu ya nchi yote; siku hiyo BWANA atakuwa mmoja na jina lake moja." Zekaria 14:9
". . . Naye akasema, Mimi ndimi Yesu. . . ." Matendo 9:5
". . . Naye ataitwa jina lake, Mashauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani." Isaya 9:5

“. . . Jina lile
lipitalo kila jina
. . . Wafilipi 2:9

JE! BIBLIA INASEMA NINI KUHUSU ONDOLEO LA DHAMBI?
". . . Mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi. . . .” Matendo 2:38
". . . Ya kwamba kwa jina lake . . . atapata ondoleo la dhambi." Matendo 10:43
". . . Watahubiriwa kwa jina lake . . . ondoleo la dhambi. . . ." Luka 24:47


JE! YESU ALIAMURU UTUMIAJI WA JINA LAKE KATIKA MPANGO WA INJILI?

". . . Na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu." Luka 24:47
". . . Mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina. . . . “ Mathayo 28:19

JE! MITUME WALIMTII?

"Petro akamwambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo mpate ondoleo la dhambi. . . . " Matendo 2:38
"Akaamuru wabatizwe kwa Jina lake Yesu Kristo. . . ." Matendo 10:48
". . . Wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu." Matendo 8:16

TUNAJIHUSISHA SISI WENYEWE NA JINA LA YESU NA KULICHUKUA JINA LAKE KWA KUTII TUNAPOBATIZWA KWA KULINGANA NA MAANDIKO.

UKWELI WA MAANDIKO:
"Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo." Matendo 4:12
"Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu...“ Wakolosai 3:17

UKWELI WA HISTORIA:
"Kanisa la mwanzo kila mara lilibatiza katika Jina la Bwana Yesu . . . ." Canney Encyclopedia. Uk. 53
"Mpangilio wa kwanza wa maneno ulikuwa ‘Katika jina la Yesu Kristo au Bwana Yesu.’" Kubatizwa katika Utatu ilikuwa tukio lililo kuja baadaye. Kamusi ya Biblia na Scribners, Uk. 241.

BASI SASA, UNAKAWILIA NINI? SIMAMA, UBATIZWE, UKAOSHE DHAMBI ZAKO, UKILIITIA JINA LAKE." Matendo 22:16



MUNGU ALIDHIHIRISHWA KATIKA MWILI


“. . . Mungu alidhihirishwa katika mwili . . . ." 1 Timotheo 3:16


· MUNGU NI WA HALI YA AINA GANI?
· YESU KRISTO ALIKUWA NANI?
· ROHO MTAKATIFU NI NANI?
· KANA UTATU (TRINITY)
HAYA NI MASWALI AMBAYO KILA MTU ANATAKIWA AYAJUE MAJIBU YAKE.


MUNGU NI ROHO! Yohana 4:24
Maandiko haya yanatusaidia kufahamu hali ya muumba wetu.

ONA UTHABITI WA MUNGU: “Ni Roho”
NENO “ROHO” LIKO KWENYE UMOJA, KUSISITIZA UKWELI KWAMBA MUNGU SI WINGI WA NAFASI.

"KUNA ROHO MMOJA!" Waefeso 4:4 MUNGU!
Kuthibitisha Marko 12:29: ". . . SIKIA, ISRAELI, BWANA MUNGU WETU NI BWANA MMOJA!"

". . . Mimi ni BWANA, Mtakatifu wenu!" Isaya 43:15

"Je! yuko Mungu zaidi yangu mimi? . . . MIMI SIJUI MWINGINE." Isaya 44:8


“MUNGU (ROHO) ALIDHIHIRISHWA KATIKA MWILI . . . ."

LINI?

* Mathayo 1:23: ". . . Imanueli; . . . Yaani, Mungu pamoja nasi."
* Waebrania 10:5: ". . . Lakini mwili uliniwekea tayari. . . ."
* Waebrania 1:3: "Yeye . . . ni . . . chapa ya nafsi yake."
* Luka 1:35: “. . . Hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu."
* Isaya 9:6: "Naye ataitwa jina lake . . . Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfame wa amani."
* Waebrania 2:16: "Maana ni hakika, hatwai asili ya malaika, ila atwaa asili ya mzao wa Ibrahimu."
* Wakolosai 2:9: "Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili."

YESU KRISTO ALIKUWA MUNGU NA PIA MWANADAMU:

KAMA MWANADAMU: ALISIKIA NJAA, KUCHOKA, AKATOA MACHOZI.

KAMA MUNGU: ALIFUFUA WAFU, AKATULIZA MAWIMBI YA BAHARI, ALISAMEHE DHAMBI.

". . . YESU HUYO . . . KUWA BWANA NA KRISTO." Matendo 2:36



KWA KUFAFANUA:


ASILI MOJA -- KATIKA HALI TOFAUTI

BABA KATIKA UUMBAJI

MWANA KATIKA UKOMBOZI

ROHO MTAKATIFU KATIKA KUZALIWA UPYA

BABA
MWANA
= HATA HIVYO NI MTU MMOJA
MUME

"... MUNGU NI MMOJA!" Wagalatia 3:20

“Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda vema. Mashetani nao waamini na kutetemeka." Yakobo 2:19

(Marejeo ya Maandiko: Kutoka 2:14-16; Kumbukumbu la Torati 6:4-6; Isaya 44:6; Isaya 45:5-6, 21-22; Isaya 48:11; Yohana 1:1-3,14; Warumi 3:30; 1 Wakorintho 1:8)


HEBU TUANGALIE KATIKA USHUHUDA WA:

MANABII:
". . . Naye ataitwa jina lake . . . Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani." Isaya 9:6
". . . Bali Bwana ndiye Mungu wa kweli; Ndiye Mungu aliye hai, Mfalme wa milele. . . ." Yeremia 10:10
". . . BWANA atakuwa mmoja . . . na jina lake moja." Zekaria 14:9

MALAIKA:
"Maana leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana." Luka 2:11

MITUME:
"Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja." Waefeso 4:5
". . . Mungu alidhihirishwa katika mwili. . . ." 1 Timotheo 3:16
"Maana katika yeye” (Yesu) “unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili." Wakolosai 2:9
"Tomaso akajibu, akamwambia, Bwana wangu na Mungu wangu!" Yohana 20:28

YESU MWENYEWE:
“Mimi na Baba tu umoja.” Yohana 10:30
“Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha. Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba?” Yohana 14:8-9
“Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. . . .” Ufunuo 1:11


MAISHA YA KIKRISTO

KUISHI KWA KITAUWA NA UTAKATIFU SHARTI UFAFANISHE MAISHA YA KILA MWAMINI

"Maana neema ya Mungu iwaokoayo … nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa." Tito 2:11-12

“Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu" 1 Petro 1:16



BIBLIA INASEMA NINI KUHUSU

DHAMBI
". . . Dhambi ni uasi." 1 Yohana 3:4
"Kila lisilo la haki ni dhambi. . . ." 1 Yohana 5:17
"Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele . . . .” Warumi 6:23
"Atendaye dhambi ni wa Ibilisi. . . " 1 Yohana 3:8

KAMA MTU ATATENDA DHAMBI MARA MOJA TU KILA SIKU NA UMRI WAKE NI:

MIAKA 20 atakuwa na dhambi 7,300
MIAKA 30 atakuwa na dhambi 10,950
MIAKA 40 atakuwa na dhambi 14,600
MIAKA 50 atakuwa na dhambi 18,250
MIAKA 70 atakuwa na dhambi 25,550
SIKU YA
HUKUMU

"Msipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake. Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia. Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele." 1 Yohana 2:15-17

UTAKATIFU NI NJIA YA MUNGU
"Tafuteni . . . utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao." Waebrania 12:14
"Lakini sasa mkiisha kuwekwa huru, na kuwa mbali na dhambi, na kufanywa watumwa wa Mungu, mnayo faida yenu, ndiyo kutakaswa, na mwisho wake ni uzima wa milele." Warumi 6:22



NENO LA MUNGU KWA AJILI YA MAISHA YETU

UPENDO:
"Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi." Yohana 13:35
"Lakini tunda la Roho ni upendo. . . ." Wagalatia 5:22

MAOMBI:
". . . Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii." Yakobo 5:16
"Ombeni bila kukoma." 1 Wathesalonike 5:17

UNYENYEKEVU:
""Nikimtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote. . . ." Matendo 20:19
"Jidhilini mbele za Bwana. . . ." Yakobo 4:10
MAZOEA
". . . Na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu." 2 Wakorintho 7:1
KUJISITIRI
"Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani." 1 Timotheo 2:9
"Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi." 1 Petro 3:3
"Wala msiifuatishe namna ya dunia hii. . . ." Warumi 12:2
KUHUDHURIA KANISANI INAVYOTAKIWA MARA KWA MARA
"Wala tusiache kukusanyika pamoja. . . ." Waebrania 10:25
UWAKILI
"Mheshimu BWANA kwa mali yako, na kwa malimbuko ya mazao yako yote." Mithali 3:9
"Siku ya kwanza ya juma kila mtu kwenu na aweke akiba kwake, kwa kadiri ya kufa nikiwa kwake. . . ." 1 Wakorintho 16:2
". . . Toa hesabu ya uwakili wako." Luka 16:2
KUTOA USHUHUDA
". . . Akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu... “ Matendo 1:8

". . . Njooni, mpatazame . . . nendeni . . .mkawaambie . . . ." Mathayo 28:6-7


KILA MTU ANATAKA:


AMANI AKILINI
"Amani nawaachieni, amani yangu nawapa . . . . sivyo kama ulimwengu utoavyo. . . ." Yohana 14:27

FURAHA
"Lakini tunda la Roho ni . . . furaha . . . ." Wagalatia 5:22
". . . Na kufurahi sana, kwa furaha isiyoneneka, yenye utukufu." 1 Petro 1:8

HERI
". . . Heri watu wenye Bwana kuwa Mungu wao." Zaburi 144:15
“Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda." Yohana 13:17



"MAANA UFALME WA MUNGU SI KULA WALA KUNYWA, BALI NI HAKI NA AMANI NA FURAHA KATIKA ROHO MTAKATIFU." WARUMI 14:17

Kuja Kwa Kristo Mara Ya Pili
"Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena. . . ." Yohana 14:3

"…Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni." Matendo 1:11

TUMAINI LILILO BARIKIWA LA MKRISTO

"Tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu." Tito 2:13



ISHARA ZA KUJA KWAKE:
"Nanyi mtasikia habari za vita na matetesi ya vita. . . ." Mathayo 24:6
Wakristo waudanganyifu. Mathayo 24:5
"... Kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali." Mathayo 24:7
"Maana watu watakuwa wenye kijipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi . . . wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu." 2 Timotheo 3:2-4
"Kwa maana kama vile ilivyokuwa siku za Nuhu. . . ." Mathayo 24:37
". . .Kama ilivyokuwa katika siku za Lutu. . . ." Luka 17:28
"Nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni." Mathayo 24:33

KUSUDI LA KUJA KWAKE:
". . . Haya, Bwana arusi. . . ." Mathayo 25:6
Yesu afananishwa na bwana arusi anayerudi kumchukua bibi arusi wake, ambaye ni kanisa lililo na JINA LAKE.
"Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo.” Yohana 14:3 (Kuwachukua watu wake mahali palipotayarishwa.)

KUWAFUFUA WENYE HAKI WALIOKUFA:
"Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. . . . “ 1 Wathesalonike 4:16-17

WAKATI WA KUJA KWAKE:
"Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye. . . ." Mathayo 24:36
"...Kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja."Mathayo 24:44

KITU MUHIMU: KUJITAYARISHA KWETU
"Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari. . . ." Mathayo 24:44

"...FANYENI BIASHARA HATA ITAKAPOKUJA." Luka 19:13


TUZO YA MILELE:

"TAZAMA, NAJA UPESI, NA UJIRA WANGU U PAMOJA NAMI. . . . ” Ufunuo 22:12
"Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu." Yohana 5:28-29
“. . . Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka.” Yakobo 4:14

HAKUTAKUWA NA WAKATI TENA

JE! KUNA NINI BAADA YA HUU MUDA MFUPI WA MIAKA MICHACHE?

WAAMINI WA KIKRISTO:
(Wanaoishi wanaodumu katika kutii na maisha ya kuridhisha.)
"Kwa maana twajua ya kuwa nyumba ya maskani yetu iliyo ya dunia hii ikiharibiwa, tunalo jengo litokalo kwa Mungu, nyumba isiyofanywa kwa mikono; iliyo ya milele mbinguni." 2 Wakorintho 5:1
"Tupate na urithi usioharibika, usio na uchafu, usionyauka, uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu." 1 Petro 1:4

KIFO: Njia nyembamba ya kuelekea uzima wa milele-- ". . . Nasi tunaona ni afadhali kutokuwamo katika mwili na kukaa pamoja na Bwana.” 2 Wakorintho 5:8
“Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya. . . .” Ufunuo 21:2


Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; . . . kwa kuwa mambo ya kwanzo yamekwisha kupita.” Ufunuo 21:4

WASIOAMINI NA WASIOTII: MUNGU HAFANYI MCHEZO NA DHAMBI!

“Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili." Ufunuo 21:8
"Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo. . . ." Ufunuo 21:27
"Na mwenye haki akiokoka kwa shida, yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi ataonekana wapi? 1 Petero 4:18

JE! MWENYE DHAMBI NI NANI?: MTU ANAYEPAKA RANGI NI MPAKA-RANGI; NA MTU ANAYECHOMEA NI MCHOMEAJI; MTU ANAYETENDA DHAMBI NI MMENYE DHAMBI!

 

 


"Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo." Luka 13:3
". . . Wakati wa kufunuliwa kwake Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika wa uweza wake; katika mwali wa moto; huku akiwalipiza kisasi wao wasiomjua Mungu, na wao wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu." 2 Wathesalonike 1:7-8

"KWA MAANA MSHAHARA WA DHAMBI NI MAUTI.” Warumi 6:23

Jehanamu ni ya moto milele usiokoma kifo ni jambo la hakika maysha ni hayana uhakika!

...Ziwa la moto... Ufunuo 19:20


KWA HIVYO UNAONA SHARTI TUFANYE UAMUZI WETU LEO!
"Tazama, wakati uliokubalika ndio sasa . . . siku ya wokovu ndiyo sasa." 2 Wakorintho 6:2

SHETANI WA KUCHELEWESHA ANAYENONG’ONEZA "BAADAYE," ANATAMANI NAFSI YAKO ILAANIWE.

UKARIBU WA MTU KWA WOKOVU HUTEGEMEA KUWA KWAKE RADHI KUKUBALI NA KUTII NENO LA MUNGU!

* UNAJALI NA NAFSI YAKO?
* UNATAKA KUOKOLEWA MILELE?
* UNGEPENDA KUMTUMIKIA NA KUMFUATA YESU?


"Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha." Mathayo 11:28 "Wote anipao Baba watakuja kwangu; wala ye yote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe." Yohana 6:37
"Tazama, nasimama mlangoni, nabisha: mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake. . . .” Ufunuo 3:20

NA TUOMBE!
"Tazama, nasimama mlangoni, nabisha: mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake. . . .” Ufunuo 3:20



MISTARI YA MAANDIKO

TOBA
Sodoma na Gomora
Yona
Yohana Mabtizaji
Yesu Kristo
Agizo Kuu
Siku ya Pentekoste
Mwanzo 19; 2 Petro 2:6; Yuda 7
Mathayo 12:41
Mathayo 3:2
Luka 13:3
Luka 24:47
Matendo 2:38

UBATIZO WA MAJI MENGI – KATIKA JINA LA YESU
Yerusalemu
Samaria
Kaisaria
Efeso
Matendo 2:38
Matendo 8:16
Matendo 10:48
Matendo 19:1,5,6

UBATIZO WA ROHO MTAKATIFU – ISHARA: WALINENA KWA LUGHA NYINGINE
Yerusalemu
Kaisaria
Ushuhuda wa Petro
Efeso
Matendo 2:4
Matendo 10:44-48
Matendo 11:15-18
Matendo 19:1, 5, 6

http://www.sayadi-al-nas.ae
http://www.sayadi-al-nas.com

صيادي الناس